Wednesday, January 8, 2014

MISS AFANYIWA KITU MBAYA NA VIBAKA, SOMA HAPA KUJUA ZAIDI

Ama kweli dunia haina huruma! Dada Happy amejikuta akiishiwa nguvu na kuanguka mbele ya kadamnasi na kuzimia pasipo msaada wowote ambapo badala yake watu waliodaiwa kuwa ni vibaka walimuibia vitu vyake vyote. 


Kwa mujibu wa mashuhuda, mrembo huyo ambaye alikuwa katika mishemishe za kawaida alidondoka ghafla akiwa Mitaa ya Nyakato jijini hapa mbele ya kituo cha polisi, Januari 4, mwaka huu.
Ilidaiwa  kuwa baada ya kupoteza fahamu, wahuni walimliza simu pamoja na fedha zote kisha kumwacha akiwa hana msaada wowote.

 Hata hivyo, dada huyo alisaidiwa na wasamaria wema ambao walimpeleka Hospitali ya Buzuruga ambapo alipatiwa matibabu na baadaye ndugu zake walipata taarifa kutoka kwa mashuhuda wanaomjua Happy kisha wakaenda kumchukua.
 Gazeti hili lilitaka kujua kilichompata mrembo huyo lakini madaktari hospitalini hapo walidai hawawezi kutoa siri ya mgonjwa huku ndugu nao wakiweka ngumu kusema kilichosababisha Happy kudondoka ghafla na kupoteza fahamu.
 “Mimi sijui kilichompata lakini sasa hivi hali ni mbaya. Unaweza ukashangaa mtu kasimama halafu akadondoka ghafla na kupoteza maisha. Cha msingi tucheki afya zetu mara kwa mara,” alisema mmoja wa ndugu hao ambaye hakutaka kutajwa gazetini.

MPENZI MSOMAJI TUPE MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII HAPA CHINI

SHARE HABARI HII KWA RAFIKI ZAKO HAPA CHINI==>>

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU BASI BOFYA "LIKE" HAPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK.

0 comments em “MISS AFANYIWA KITU MBAYA NA VIBAKA, SOMA HAPA KUJUA ZAIDI”

Post a Comment

 

Mambomseto Blog Copyright © 2011 -- Template created by SKENDO TEAM -- Powered by SKENDO TEAM

Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter