Wednesday, January 22, 2014

EMMANUEL MSUYA (MSHINDI WA BSS 2013 ) AONYESHA ALICHOFANYA NA ZILE MILLION 50 ALIZOSHINDA

Emma Msuya (mwenye shati jekundu)  Nov 30, 2013, siku aliyotangazwa mshindi wa zile milioni 50 za mshindi wa Epiq Bongo Star Search.


Nyumba na gari ya Emmanuel Musuya mshindi wa BSS 2013 
Studio ya Emmanuel Msuya


Blogger Tricks

Tuesday, January 21, 2014

LAANA HII: WAKUTWA WAKILA URODA MAKABURINI. WAKAMATWA NA KUCHARAZWA VIBOKO..!!


Wawili wakutwa maeneo ya makaburini wakila uroda, walikamatwa na kucharazwa viboko hadi kuvimba miili yako. na baadae kuomba msamaha kwa kitendo hicho.

DIVA, B 12, MCHOMVU WARUDISHWA KAZINI CLOUDS

WATANGAZAJI maarufu Bongo wa Redio Clouds Fm ya jijini Dar es Salaam, Hamis Mandi ‘B 12’, Adam Mchomvu na Loveness Malinzi ‘Diva’, wamerudishwa kazini baada ya kuomba msamaha.

Watangazaji hao walisimamishwa na uongozi wa Clouds baada ya kuchoshwa na tabia yao ya utovu wa nidhamu hivi karibuni. 

HAWA NDIO MAWAZIRI WALIOPIGWA CHINI BILA YA KUTEGEMEA BAADA YA UTEUZI WA BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI

Juzi Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sifue kwa niaba ya Rais Jakaya Kikwete alitangaza mabadiliko katika baraza la mawaziri ambapo ‘jiwe’ limetua kwa wasiotegemea.
Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sifue (kushoto) akitangaza Baraza jipya la Mawaziri.
Katika mabadiliko hayo wizara tano zimepata mawaziri wapya kujaza nafasi za waliovuliwa nyadhifa zao kutokana na kashfa ya Operesheni Tokomeza.
Waliochakuliwa ni Mathias Chikawe aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Hussein Mwinyi aliyepelekwa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Lazaro Nyalandu amepewa Wizara ya Maliasili na Utalii kuiongoza.
Wengine ni Saada Mkuya Salum, ataongoza wizara ya fedha ambapo Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi mpya ni Dr. Titus Kamanyi. Naye Asha Rose Migiro ameteuliwa kuwa Waziri wa Sheria na Katiba.
Manaibu mawaziri walioteuliwa na wizara zao kwenye mabano ni Adamu Malima (Fedha), Amos Makalla (Maji), Jonister Mhagama (Elimu), Janet Mbene, (Viwanda na Biashara), Kaika Telele (Mifungo, Uvuvi), Kwebe Steven Kwembe ( Jinsia na watoto) na Charles Kitwanga (Nishati).
Hata hivyo, Naibu Waziri wa Elimu, Philip Mulugo amejikuta akitupwa nje ya wizara hiyo na hakuambulia nafasi yoyote.


UKATILI WA KUTISHA BABA WA KAMBO AWACHOMA MOTO WATOTO WAWILI HUKU MAMA YAO AKISHANGILIA ,KISA KUTUMIA TSH 10,000 VIBAYA....MATUKIO KATIKA PICHA

Askari  polisi akimuongoza mama  wa watoto hao polisi
Askari  wanaharakati  wa dawati la mtandao wa jinsia kulia na kushoto wakiwa  wamemkamata mama wa watoto  hao tayari kwenda polisi
Hapa wakiingia na mama  huyo katika ofisi za dawati la jinsia mkoa wa Iringa
Hivi  ndivyo  watoto  hao  walivyougunzwa  kinyama na baba wa kambo 



Mrakibu mwandamizi  wa  polisi na mkuu  wa dawati la jinsia na  watoto mkoa  wa Iringa ,Atupele Mwambunda  akiwatazama  watoto hao nje ya ofisi ya  dawati la jinsia mkoa  wa Iringa
Mama  wa  watoto hao  Watende  Sanga  akiendelea  kupika chakula baada ya  watoto kuchukuliwa na polisi

Askari  wa dawati la jinsia  Iringa akiingia kumsimamia  mama wa watoto hao kufunga duka lake kabla ya kuchukuliwa kwenda  polisi


 Mkuu  wa dawati la jinsia mkoa wa Iringa Atupele Mwambunda (kulia) akimhoji  mama wa  watoto hao Watende Sanga kuhusiana na ukatili  uliofanywa dhidi ya  watoto  wake.
.................................................................................................
WAKATI  wanaharakati  mbali  mbali wakiwemo  wanaharakati  wa mtandao wa kijinsia  Tanzania (TGNP)  ,wanaharakati  wa  haki za binadam,WAMA kuendelea  kukemea na kuendelea  kupinga vikali vitendo vya  ukatili wa kijinsia na uyanyasaji wa  wanawake na watoto hata kulifanya jeshi la jeshi la  polisi  kuanzisha dawati maalum  linaloshughulikia vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia ,baba  wa kambo Mussa Mdetela aamua kuwatesa kinyama watoto wake kwa kuwachoma moto miguu  wakituhumiwa kuiba Tsh 10,000
Wakizungumza  kwa shida na mtandao  huu  watoto hao Baraka Rajab Mohamed anayesoma darasa la kwanza na Mood Rajab Mohamed   anayesoma  darasa la sita walisema kuwa  ilikuwa ni siku ya tarehe 3 ambapo walichukua pesa hiyo kiasi cha Tsh 10,000 na kwenda kununua chakula baada ya  mama yao kushindwa kuwaandalia chakula.
Hata  hivyo Mood anayesoma darasa la sita  msingi Lugalo  alisema kuwa siku ya  tukio mdogo  wake  alikwenda ndani na kuchukua  kiasi hicho cha fedha na baada ya muda  walishirikiana katika matumizi .
Watoto  hao ambao wanadai kuwa baba  yao mzazi  Rajab Mohamed aliwaacha na sasa anaishi  jijini Dar es Salaam na wao  wamekuwa  wakiishi na baba yao mdogo huyo ambae  mara kwa mara amekuwa  akiwaadhibu vikali.
Kwani  walisema  kuwa kutokana na mara kwa mara kushinda bila kula ndipo siku  hiyo walipoamua kuchukua pesa  hiyo ili kununua bagia na vitumbua ili kujikimu kwa njaa .
Hata  hivyo  walisema baada ya  baba yao kurudi kutoka katika shughuli zake na kubaini kuwa  fedha  hiyo imechukuliwa ndipo alipowakamata na kuwafunga kamba na kuanza kuwatesa kwa kichapo ili waweze  kusema mtu aliyechukua pesa  hiyo.
“Alitufunga kamba miguuni na mikononi na kuanza kututesa kwa kutupiga na baada ya kuona hatusemi ndipo alipochukua makaratasi ya naironi na kutufunga miguuni kisha kuchukua kiberiti ,mafuta ya taa na kuwasha  moto katika miguu yetu huku akiendelea  kutupiga na moto ukiwaka miguuni….wakati huo mama alikuwa amekaa mlangoni akishangilia kuwa wapige sana mimi  nimewachoka hawa watoto heri wafe tu” walisema watoto hao
Atupele Mwambunda mkuu wa dawati la jinsia mkoa  wa Iringa ameuthibitishia mtandao  huu juu ya tukio  hilo na kuwa kitendo hicho ni cha kinyama na kamwe hakitavumilika.
Alisema kuwa  kuanzishwa kwa dawati hilo ni kutaka kukomesha  vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kama  hivyo na kuwataka  wazazi na jamii kuepuka kuchukua sheria mkononi kwa  kuwatesa  watoto kama hao ambao mwisho  wa  siku  wanapoteza mwelekeo wa maisha.
Mwambunda  alisema  kuwa hadi sasa wamefanikiwa  kumkamata mama  wa watoto hao Watende  Sanga huku  mzazi  mwenzake Mussa Mdetele bado anatafutwa  na jeshi la  polisi ili  kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kuwatesa  watoto hao.
Huku mama  wa watoto hao  akidai  kuwa wakati baba yao mdogo akiwapiga watoto hao yeye hakujua kinachotokea  japo alikuwa na taarifa ya  kupotea kwa  pesa katika duka na kuwa baada ya tukio hilo aliwanunulia dawa ili kuwatibu  kinyemela pamoja na kuwaombea  ruhusa shuleni .
Pia mwanamke  huyo aliomba  kusamehewa kwa madai  kuwa hakujua kama kushangilia wakati  baba yao akiwatesa  watoto hao ni kosa

SOMA ALICHOKISEMA TUNDA MAN KUHUSU YEYE NA ROSE NDAUKA KATIKA MAHUSIANO YA KIMAPENZI

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Tunda Man, amesema mpenzi wake wa kwanza katika maisha yake ni mwanadada muigizaji wa filamu nchini Rose Ndauka,ambaye waliachana tangu 2006.
Akizungumza na XXL ya Clouds Fm leo Tunda amesema walikuwa wakikutana na mwanadada huyo katika studio moja huko kariakoo hali iliyowapelekea kuanza mahusiano yao yamapenzi.
“Kuna studio moja kariakoo,wanadada walikuwa wanakuja kuchana na yeye anakuja studio anaangalia situation zinavyoenda, kwahiyo kuanzia hapo ndiyo akaanza kunijua nini, nikaenda kwao kila kitu kikawa fresh kila kitu kikawa kinaenda poa ni 2006 kitu kama hicho, yani tumeachana kabla, hamna hata mmoja aliyekuwa star, sasa tumejikuta kila mmoja anafanya issue zake na mimi nafanya issue zangu, mpaka sasa hivi nikikutana nae, nasikia ameolewa peace tu ,kama na shida na yeye kwasababu na yeye sasa hivi anapiga mapigo ya movie na mimi na movie zangu kama vipi namdondosha halafu namlipa”, alisema Tunda

MWENDELEZO WA MASSAGE NA MAMBO YA AIBU YA MTANZANI "CHAGA BARBIE" AKIMCHANA NA KUMUAIBISHA MPENZI WAKE PREZZO

Prezzo na StarlishaLile penzi la mkali kutoka Kenya Prezzo na mdada kutoka uchagani Chagga Barbie limeota mbawa na hatimaye kilichofata ni matusi kuwekeana mambo hadharani bila hata aibu, Mdada ameamua kumwaga kila kitu hadharani na hapo chini ni kila kitu alichoongea mwanadada kutoka TZ aishie USA.
 Swahilitz imefatilia mkasa huu na tumeona sio mbaya tukakuwekea picha hapa uone jinsi mdada alivyofunguka vya kutosha. 














 

Mambomseto Blog Copyright © 2011 -- Template created by SKENDO TEAM -- Powered by SKENDO TEAM

Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter