Wednesday, January 8, 2014

NI NOUMA....JOHARI APOMBEKA KUFURAHIA RAY KUPIGWA CHINI...

Blandina Chagula ‘Johari’.
STAA wa kitambo kwenye filamu za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amenaswa akipiga mitungi kwa sana ikiwa ni sehemu ya kufurahia uongozi mpya wa Klabu ya Bongo Movie Unity.
Tukio hilo lilitokea wikiendi iliyopita katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, Dar ambapo uchaguzi wa safu mpya ya uongozi wa klabu hiyo ulimalizika na matokeo kuwatangaza mwenyekiti mpya Steven Mengele ‘Nyerere’ na wenzake kuwa washindi.

Katika mahojiano na mwandishi wetu, Johari alisema: “Kwa upande wangu ninawaamini viongozi wote waliochaguliwa katika kutuletea maendeleo katika klabu yetu kwa kufanya kazi kwa umoja na mshikamano. Wote nawaamini na kusema kweli, hawa ndiyo viongozi tuliokuwa tunawataka.”
Katika uchaguzi huo, nafasi ya Makamu Mwenyekiti ilikwenda kwa Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’, Katibu Mkuu Willium Mtitu, Katibu Msaidizi Devotha Mbaga, Mweka Hazina Issa Mussa ‘Cloud’ na msaidizi wake Sabrina Rupia ‘Cathy’.


MPENZI MSOMAJI TUPE MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII HAPA CHINI

SHARE HABARI HII KWA RAFIKI ZAKO HAPA CHINI==>>

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU BASI BOFYA "LIKE" HAPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK.

0 comments em “NI NOUMA....JOHARI APOMBEKA KUFURAHIA RAY KUPIGWA CHINI...”

Post a Comment

 

Mambomseto Blog Copyright © 2011 -- Template created by SKENDO TEAM -- Powered by SKENDO TEAM

Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter