Friday, January 10, 2014

SANDRA NA RUSHWA YA NGONO BONGO MOVIE

STAA wa filamu Bongo, Salma Salmini ‘Sandra’ amesema kuwa tangu ajiunge Bongo Movie hakuna manufaa aliyoyapata kwa kuwa chama hicho kinaendekeza ubaguzi kwa kuthamini rushwa ya ngono.
Salma Salmini ‘Sandra’.
Akipiga stori na paparazi wetu alisema, kikubwa kinachoikwamisha tasnia hiyo ambayo kwa sasa inaongozwa na Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ ni watu kusaidiana wenyewe kwa wenyewe kwa kuwa labda wanatoka kimapenzi au kutegemea kupewa rushwa ya ngono ili impe shavu mtu.
“Namsihi sana huyu kiongozi wetu wa sasa awe makini na hili suala, yeye pamoja na utawala wake wote wapinge haya mambo na tushikamane ile kuleta maendeleo, maana kila siku wanaopewa madili ya maana ni walewale lakini wengine tunaheshimika kwa majina tu huku dhiki zikitutawala,” alisema Sandra.


MPENZI MSOMAJI TUPE MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII HAPA CHINI

SHARE HABARI HII KWA RAFIKI ZAKO HAPA CHINI==>>

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU BASI BOFYA "LIKE" HAPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK.

0 comments em “SANDRA NA RUSHWA YA NGONO BONGO MOVIE”

Post a Comment

 

Mambomseto Blog Copyright © 2011 -- Template created by SKENDO TEAM -- Powered by SKENDO TEAM

Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter